Synopsis
Listen to interviews, features and community stories from the SBS Radio Swahili program, including news from Australia and around the world. - Sikiza mahojiano, makala na hadithi za jumuiya kutoka Idhaa ya Kiswahili ya SBS Radio, ikijumuisha taarifa za habari kutoka Australia na ulimwenguni.
Episodes
-
Taarifa ya Habari: Sussan Ley astaafu kutoka siasa
13/02/2026 Duration: 14minKiongozi wa upinzani wa kwanza wa kike nchini Australia Sussan Ley ametangaza kuwa amestaafu kutoka siasa.
-
Australia yafafanuliwa: Jinsi yakupona kutokana na moto wa vichaka
13/02/2026 Duration: 15minHali ya mazingira ya joto na ukavu pamoja na mandhari yakipekee, hufanya Australia iwe mojawapo ya nchi zinazo kabiliwa na moto wa vichaka zaidi duniani.
-
Taarifa ya habari:Ziara ya rais wa Israel Isaac Herzog, yazua utata
10/02/2026 Duration: 12min**ZIARA YA RAISI WA ISRAEL AUSTRALIA YAZUA UTATA HUKU WAANDAMANAJI NA POLISI WAKIKABILIANA KATIKA MAANDAMANO DHIDI YA RAIS HUYO ** SERIKALI YAZINDUA MPANGO WA KWANZA WA FAMILIA NA UNYANYASAJI WA WANAWAKE NA WATOTO WA MATAIFA YA KWANZA. **NA CHAMA CHA LIBERAL BADO LIANENDELEA KUWA NA MZOZO WA UONGOZI WA CHAMA BAADA YA KUGAWANYIKA KWA SIKU 17
-
Yaliyojiri Afrika:Rwanda haikubali kutishwa na Marekani
10/02/2026 Duration: 07minKwa habari na melezo zaidi, tembelea tovuti ya sbs.com.au.
-
What actually happened on January 26? - Australia yafafanuliwa:Nini kilifanyika Januari 26?
10/02/2026 Duration: 08minJanuary 26 is one of the most debated dates in Australia’s history. Often described as the nation’s birthday, the day marks neither the formal founding of the colony nor the creation of the Commonwealth. Instead, it reflects a layered history shaped by colonisation, political decisions, and ongoing First Nations resistance. Understanding what actually happened on January 26 reveals why the date is experienced so differently across the country. - Tarehe 26 Januari ni moja ya tarehe zinazojadiliwa sana katika historia ya Australia. Mara nyingi inatajwa kama siku ya kuzaliwa ya taifa, lakini siku hiyo haimaanishi kuundwa rasmi kwa koloni au kuanzishwa kwa Jumuia. Badala yake, inaakisi historia yenye tabaka nyingi inayoundwa na ukoloni, maamuzi ya kisiasa, na upinzani unaoendelea wa Mataifa ya Kwanza. Kuelewa kilichotokea hasa tarehe 26 Januari kinafunua ni kwa nini tarehe hiyo inaathiriwa kwa namna tofauti katika nchi nzima.
-
Makala leo:Australia na Indonesia wasaini mkataba wa usalama
09/02/2026 Duration: 08minWaziri Mkuu Anthony Albanese amepongeza makubaliano mapya ya usalama na Indonesia kama mabadiliko muhimu kuelekea ushirikiano wa karibu wa ulinzi kati ya nchi hizi mbili. Hata hivyo, wachambuzi wanaonya kwamba mkataba huo unaweza kuja na gharama kubwa, ikiwezekana kupuuza masuala ya haki za binadamu yanayoendelea huko Papua Magharibi na wasiwasi kuhusu mwelekeo wa kisiasa wa siku zijazo wa serikali ya Indonesia
-
Makala leo:Shirika la Haki za Binadamu laonya kuwa demokrasia iko hatarini ikilinganishwa na miaka ya 1980
09/02/2026 Duration: 10minDemokrasia na utaratibu wa kimataifa unaozingatia sheria ziko hatarini, kulingana na ripoti ya kila mwaka ya Shirika la haki za binadamu ama Human Rights Watch. Kuna msisitizo mahususi juu ya Marekani na kile ambacho chombo cha kimataifa kinaelezea kama kudorora kwa haki za binadamu, lakini pia kuna tahadhari juu ya Australia. Sera za uhamiaji na kuwekwa kizuizini kwa vijana za Australia zinaorodheshwa kama 'mapungufu makubwa', zikionyeshwa kuwa ni demokrasia pekee ya Magharibi isiyo na sheria ya kitaifa ya haki za binadamu.
-
Taarifa ya habari:waziri Mkuu Anthony Albanese atasaini mkataba wa kihistoria wa usalama na Rais wa Indonesia
06/02/2026 Duration: 12min**WAZIRI MKUU ANTHONY ALBANESE YUKO INDONESIA KUSAINI MKATABA WA KIHISTORIA WA USALAMA **MAJESHI YA MAREKANI NA URUSI YATANGAZA KUANZA KUSHIRIKIANA TAARIFA ZA KIJESHI HUKU MAZUNGUMZO YA AMANI NA UKRAINE YAKIENDELEA **WATU ZAIDI YA MIA MOJA HAMSINI WAFARIKI BAADA YA SHAMBULIO NIGERIA
-
Yaliyojiri Afrika: AL Islam Gaddafi, mwanawe Omar Gaddafi, auwawa
06/02/2026 Duration: 08min*AL-Islam Gaddafi auwawa Libya *Vikwazo vimewekwa na Marekani dhidi ya watu wanaodaiwa kuchochea vita Sudan
-
Makala leo:viwango vya riba vyaongezeka baada ya kusitishwa kwa miaka miwili
06/02/2026 Duration: 06minBenki ya Hifadhi ya Australia imehitimisha mapumziko ya miaka miwili kwa kuongeza viwango vya riba hadi asilimia 15, jambo ambalo limeanzisha mjadala mkali wa kisiasa juu ya kama matumizi ya serikali au mahitaji ya watu binafsi ndiyo yanayosababisha mfumuko wa bei kuendelea. Wakati Mweka Hazina anatetea bajeti na kuashiria mashinikizo ya nje, Upinzani na Kijani wanadai kuwa sera za sasa zinawaadhibu Waustralia wa kawaida na zinaacha mbali njia zingine za kiuchumi.
-
Makala leo:Utafiti umebaini ongezeko la upekuzi usio na kibali katika jamii zenye tamaduni mbalimbali
06/02/2026 Duration: 04minUtafiti mpya unaonyesha kuwa jamii zilizo na mchanganyiko wa rangi tofauti zinafanyiwa upekuzi bila kibali mara tatu na nusu zaidi kuliko jamii katika maeneo yenye watu wengi weupe. Kulingana na uchambuzi wa matumizi ya nguvu za upekuzi zisizo za kawaida na Polisi wa Victoria, hali hii inaonekana hata pale ambapo maeneo ya jamii zenye watu wengi weupe yana viwango vya juu vya uhalifu.
-
How does IVF work in Australia? - Australia yafafanuliwa:IVF hufanyaje kazi nchini Australia?
05/02/2026 Duration: 08minDid you know that IVF is not the first, but in fact the last step in a sequence of fertility treatments? In Vitro Fertilisation is regulated by state and territory laws. It can also be expensive and emotionally challenging. Here’s what to expect when aiming to start a pregnancy with IVF in Australia. - Je, mnajua kwamba IVF si hatua ya kwanza, bali ni hatua ya mwisho katika mlolongo wa matibabu ya uzazi? Uliopo wa Mbolea ya Nje ya Mwili unasimamiwa na sheria za mitaa na eneo. Pia inaweza kuwa ghali na pia ngumu kihisia. Hiki ndicho mnachopaswa kutegemea ama kuzingatia mkitaka kuanzisha ujauzito kwa kutumia IVF nchini Australia.
-
Makala leo:Mildura imevunja rekodi ya joto kali,mabadiliko ya hali ya hewa yanapoendelea,nini kinafuata?
05/02/2026 Duration: 13minKwa wengi katika kusini-mashariki mwa Australia, siku baada ya Siku ya Australia ilileta hali ya joto kali na rekodi za viwango vya joto. Katika Mildura, jimboni Victoria, kaskazini-magharibi zaidi, joto lilifikia nyuzi 48.6. Na wakati maeneo ya pwani yalifurahia kupungua kwa joto, maeneo ya bara yalilazimika kukabiliana na joto kali lililodumu kwa wiki moja. Wataalamu wanasema aina hizi za matukio zitaendelea kuongezeka kwa wakati kutokana na athari za mabadiliko ya tabianchi - lakini wakati kumejaa habari nyingi kuhusu jinsi hiyo inaathiri vituo vya mijini, maeneo ya vijijini nchini Australia hayajapata umakini sawa. SBS ilitembelea Mildura kuona jinsi eneo hilo lilivyohisi joto, na wanavyofanya kukabiliana na mabadiliko ya hali ya hewa katika ngazi ya eneo hilo.
-
Taarifa ya habari:Benki ya hifadhi inatarajiwa kuongeza kiwango cha riba
03/02/2026 Duration: 11min**BENKI YA HIFADHI INATARAJIWA KUONGEZA KIWANGO CHA RIBA **INDIA NA MAREKANI WAMEFIKIA MAKUBALIANO YA KIBIASHARA **KITUO CHA KITAIFA CHA DAWA ZA KULEVYA CHATOA TAHADHARI KUHUSU DAWA HATARI ZA STAREHE ** IRAN INAJIANDAA KWA MAZUNGUMZO NA MAREKANI KUHUSU NYUKLIA
-
Yaliyojiri Afrika:Marekani kutathmini upya ushirikiano wake na Uganda baada ya uchaguzi
02/02/2026 Duration: 08minKwa maelezo ama habari zaidi elekea kwenye tovuti yetu ya sbs.com.au/swahili.
-
Makala leo:mkataba wa muungano wa falepili kati ya australia na tuvalu wazinduliwa rasmi
02/02/2026 Duration: 06minMkataba wa Muungano wa Falepili kati ya Australia na Tuvalu uliangaziwa kama wa kwanza wa aina yake duniani, ukiwa na kifungu kimoja cha makubaliano kinachoruhusu hadi watu 280 wa Tuvalu kuhamia Australia kila mwaka kama njia ya kukabiliana na viwango vya bahari vinavyoongezeka na kutishia ardhi yao. Kikundi cha kwanza cha wahamiaji chini ya makubaliano haya sasa wamewasili Australia. Hata hivyo, pamoja na kuwepo kwa jamii ndogo ya watu wa Tuvalu huko, wanakabiliwa na changamoto ya kuzoea makazi mapya, huku wakidumisha uhusiano na jamii na utamaduni wao.
-
#102 Getting organised (Med) - #102 Jinsi ya kujipanga
02/02/2026 Duration: 10minLearn practical English phrases for getting organised and managing daily tasks, including planning ahead, meeting deadlines, and staying on top of responsibilities. - Jifunze misemo ya Kiingereza kwa vitendo ili kujipanga na kusimamia majukumu ya kila siku, ikiwemo kupanga mapema, kufikia tarehe za mwisho, na kuwajibikia majukumu yenu.
-
#101 Having a laugh (Med) - #101 Jinsi tofauti ya kuelezea kicheko
02/02/2026 Duration: 11minLearn how to talk about things that make you laugh. Practise phrases that help you share stories, react to jokes, and enjoy conversations more. - Jifunze jinsi ya kuzungumzia mambo yanayowachekesha. Fanyeni mazoezi ya misemo inayowasaidia kushiriki hadithi, kuitikia vichekesho, na kufurahia mazungumzo zaidi.
-
Public transport in Australia: breaking down the basics - Australia yafafanuliwa:mambo ya msingi kuhusu usafiri wa umma nchini Australia
30/01/2026 Duration: 08minLike in most countries, public transport in Australia is the cheapest way to get around. It includes trams, buses, trains and ferry services. And each state or territory has its own transport network. However, navigating Australia’s public transport system with ease requires knowing the basics around how it works and what to expect. - Kama ilivyo katika nchi nyingi, usafiri wa umma nchini Australia ni njia ya bei nafuu zaidi ya kusafiri. Unajumuisha tramu, mabasi, treni, na huduma za feri. Kila jimbo au eneo la nchi lina mtandao wake wa usafiri. Hata hivyo, kuzunguka kwa urahisi katika mfumo wa usafiri wa umma wa Australia kunahitaji kujua mambo ya msingi kuhusu jinsi unavyofanya kazi na nini cha kutarajia.
-
Taarifa ya habari:tahadhari ya jua na joto kali iliyovunja rekodi yaendelea kutolewa
30/01/2026 Duration: 11min**WATU WAWILI WAKAMATWA NA POLISI BAADA YA TUKIO LA UFYATULIAJI RISASI HUKO GEELONG. **KIPITO CHA RAFAH KATI YA EGYPT NA GAZA KUFUNGULIWA BAADA YA MIAKA MIWILI ** TAHADHARI KUHUSU MLIPUKO WA VIRUSI VYA NIPAH HUKO INDIA.